Recent Posts

KWA MATANGAZO WASILANA NA UONGOZI WA Deopa TV NO:0765-743393 AU 0658508231, EMAIL:deostivu123@gmail.

MICHEZO

MANCHESTER WAONESHA UBABE WAO DHIDI  WAICHAPA



Manchester United imezidi kuonesha ubabe wake kwa Liverpool, baada ya kuitandika mabao 2-1 kwenye Uwanja wa Old Trafford leo, mechi ya Ligi Kuu England.

United imepata mabao yake kupitia Marcus Rashford, aliyefunga katika dakika za 14 na 24 kipindi cha kwanza.

Hadi dakika 45 za awali zinamalizika, United ilikuwa mbele kwa mabao 2-0.

Licha ya kutawala kwa asilimia kubwa katika dakika zote 90, Liverpool ilifanikiwa kupata bao la kufutia machozi baada ya Eric Bailly kujifunga ikiwa ni dakika ya 66, baada ya kushindwa kuokoa mpira a krosi uliopigwa na Sadio Mane.

United sasa imeendelea kusalia nafasi ya pili ikiwa na alama 65 dhidi ya Liverpool yenye 60.
follow my blogy  deopa tv







 Ligi kuu ya Vodacom Tanzania Bara kupigwa wikiendi hii

 Ligi kuu ya Vodacom Tanzania Bara kupigwa wikiendi hii
Mzunguko wa 22 wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara unaendelea wikiendi hii Machi 11, 2018 kwa kuchezwa mechi tano (5).

Mechi mbili za mzunguko huo zilizokuwa zichezwe Machi 11, 2018 zimebadilishiwa Simba SC waliokuwa wacheze ugenini dhidi ya Njombe Mji mchezo huo sasa utapangiwa tarehe nyingine baada ya wekundu hao wa Msimbazi kuomba kusogezwa mbele ili kupata muda wa maandalizi yao ya marudiano dhidi ya Al Masry Kombe la Shirikisho utakaochezwa Port Said nchini Misri Machi 17, 2018.
Mchezo wa Kagera na Mwadui uliokuwa uchezwe Machi 11, 2018 kwenye Uwanja wa Kaitaba sasa utachezwa Jumanne Machi 13, 2018 kutokana na kusogezwa kwa mechi yao dhidi ya Young Africans uliyochezwa jana Machi 9, 2018.
Mechi nyingine za mzunguko wa 22 zitakazochezwa Jumapili Machi 11, 2018
AzamFC  vs Mbao FC (Azam Complex,Chamazi)
Ruvu Shooting vs Mbeya City (Mabatini)
Singida United vs Ndanda  (Namfua)
Majimaji vs Lipuli (Majimaji)
Tanzania Prisons vs Mtibwa Sugar (Sokoine)





1 comment: