Rais Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. John Pombe
Magufuli amemuagiza Waziri wa TAMISEMI kuwasimamisha kazi Wakurugenzi wa
Halmashauri ya Kigoma Ujiji na Pangani kutokana na Wilaya zao kuwa na
hati chafu.
Rais Magufuli amewasimamisha kazi Wakurugenzi hao leo Ikulu jijini
Dar es salaam, baada ya kupokea ripoti ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa
hesabu za serikali(CAG), Profesa Mussa Assad.
“Wakurugenzi wa Halmashauri ya Kigoma Ujiji na Pangani wameandikiwa
hati chafu, inabidi tuanze kuchukua hatua.Ninawasimamisha mara moja
Wakurugenzi wa halmashauri hizi mbili kwa Waziri wa TAMISEMI yuko hapa
kwahiyo Wakurugenzi wa wilaya hizo wasimamishwe kazi leo, inawezekana si
vizuri sana ila inabidi tuchukue hatua,“ amesema Rais Magufuli.
Prof. Assad amesema serikali za mitaa 140 zilishindwa kukusanya
mapato ya shilingi bilioni 116 ambazo ni sawa na mapato ya asilimia 22
ya mapato yake.
No comments:
Post a Comment