Recent Posts

KWA MATANGAZO WASILANA NA UONGOZI WA Deopa TV NO:0765-743393 AU 0658508231, EMAIL:deostivu123@gmail.

Kesi ya Aveva, Godfrey Nyange Kaburu zapigwa kalenda

Kesi inayowakabili viongozi wa klabu ya Simba SC, Evans Aveva na Godfrey Nyange Kaburu imehairishwa mpaka  Aprili 12  mwaka 2018.

Rais wa Simba SC, Aveva ambaye anasumbuliwa na maradhi kwa muda mrefu amefika katika mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu kuhudhuria kesi yake inayomkabili ambapo jana alipaswa kusomewa maelezo ya awali na mwenzake mbele ya Hakimu Mkazi Mkuu, Thomas Simba.
 
Licha ya kusomewa maelezo hayo, kesi hiyo imeahirishwa tena mpaka Aprili 12  mwaka 2018 kufuatia Wakili wa TAKUKURU, Leonard Swai, kuomba hati ya mashtaka ifanyiwe mabadiliko.
 
Swai ameiomba Mahakama kubadilisha hati ya mashtaka kwa kumuongeza mshtakiwa mwingine ambapo Aprili 12 mwaka 2018 watasomewa maelezo hayo ya awali.
 
Taarifa zinaeleza kuwa hatua hiyo imefikia hapo baada ya upelelezi kukamilika upande wa mashtaka.
Mhusika mwingine anayekabiliwa na kesi hiyo ni Makamu wa Rais wa Simba, Godfrey Nyange Kaburu ambaye alitinga pia mahakamani hapo leo.
 
Washtakiwa wote wawili wanakabiliwa na mashtaka matano ya kughushi nyaraka za uongo na utakatishaji wa fedha, kiasi cha USD 300,000.

No comments:

Post a Comment