Msanii wa Bongo Fleva, Sam wa Ukweli amefariki dunia usiku wa kuamkia Juni 7, 2018 baada ya kuumwa na mwili wake kupelekwa katika hospital ya Mwananyamala.Pia, aliyekuwa mtayarishaji wa nyimbo za Sam wa Ukweli, Steve amesema Sam alikuwa akiumwa na walipomuuliza alisema ni UKIMWI wa kulogwa.R. I .P SAM WA UKWELI
Taarifa hiyo imethibitishwa na msambazaji wa nyimbo zake na Meneja wa ‘Team Mtaa kwa Mtaa’, Amri the Business ambaye aneeleza kwa masikitiko makubwa kuwa Sam amefariki dunia na kumtakia kupumzika kwa amani.
“Siamini kilichotokea muda huu ila sina jinsi, kwani woote safari ni moja, pumzika kwa amani Sam wa Ukweli, hakika nilikupenda kama ndugu yangu wakuzaliwa tumbo moja" amesema Amri the Business.
TUTAKUKUMBUKA
No comments:
Post a Comment